Shirika la Habari za Maendeleo Tanzania (TADIO) limeanza kusambaza vifaa vya kujikinga na magonjwa ya mlipuko vilivyotolewa na UNESCO kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kwa vituo vya redio jamii chini ya mwamvuli wa TADIO.Vifaa hivi vyenye thamani zaidi ya TZS milioni 10 vinakusudiwa kufikia zaidi ya watendaji 300 wa redio na kusaidia waandishi wa habari kutoka vituo hivyo kujikinga na magonjwa ya milipuko katika shughuli zao za kila siku.

Wakati wa makabidhiano, mwenyekiti wa TADIO, Bwana Prosper Kwigize aliwataka mameneja wa redio wanachama wa TADIO kuhakikisha kuwa vifaa hivyo vinatumika vizuri na vinamfikia mtumiaji wa mwisho ambaye ni mwandishi wa habari haswa waandishi wa habari wanawake.

Mameneja wa redio wanachama wa TADIO waliishukuru UNESCO na TADIO kwa msaada unaojali usalama wa wanahabari wa redio zao na waliahidi kuwa vifaa hivyo vitatumika kama ilivyokusudiwa.
Tazama picha zaidi hapo chini:
Meneja wa Mazingira FM, Bw. Ally Nyamkinda akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Redio Jamii FM, Bw. Amua Rushita akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Nuru FM, Bw. Victor Chakudika akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Chai FM, Bw. Ally Malwenga akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Ileje FM, Bw. Maoni Mbuba akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Kaimu Meneja wa Uyui FM, Bi. Nyamiz Mdaki akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Dodoma FM, Bi. Zania Miraji akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Huheso FM, Bi. Chevawe Mandari akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Sibuka FM, Bw. Daniel Manyanga akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Mpanda Radio FM, Bw. Alinanuswe Edward akikabidhiwa vifaa vya kujikikinga na magonjwa ya mlipuko na Mwenyekiti wa TADIO, Bw. Prosper Kwigize Vifaa vya kujikinga na magonjwa ya mlipuko vikiwa vimewasili Jamii FM, Mtwara