Machweo nyuma ya majengo.

TANZANIA YATANGAZA WAGONJWA WAPYA 53 WA CORONA

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema idadi hiyo imefikiwa baada ya Wagonjwa wapya 53 kukutwa na #COVID19

Wagonjwa wote ni Watanzania ambapo 38 wanatoka Dar; 10 wanatoka Zanzibar; Kilimanjaro 1; Mwanza 1; Pwani 1; Lindi 1 na Kagera 1

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ametoa idadi hiyo huku akisema Wagonjwa 4 wanapatiwa matibabu ya Wagonjwa mahututi kutokana na kusumbuliwa na matatizo mengine ya kiafya

Aidha, wagonjwa 131 wanaendelea vizuri na tayari Wagonjwa 11 wamepona maambukizi ya corona

Wananchi wenye dalili za ugonjwa huo wametakiwa kuacha kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili na badala yake Serikali imeamua kutumia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Amana kama Kituo maalum cha matibabu ya Ugonjwa wa corona

Serikali imesema hospitali hiyo ndiyo hospitali kuu ya rufaa ya Kitaifa, ina wagonjwa wengine na pia ndio inatoa matibabu mengine ikiwemo upasuaji wa figo, moyo, mifupa na mishipa ya fahamu