Machweo nyuma ya majengo.

WAANDISHI WA HABARI WAFANYA ZIARA  MAKAO MAKUU YA IDARA YA HABARI MAELEZO

 

Picha ya pamoja ya Waandishi wa habari kutoka radio 18 za kijamii wanachama wa TADIO wakiwa na Kaimu mkurugenzi wa Idara ya Habari maelezo aliyevaa Suti bwana Rodyne Mbuya kulia kwake Prosper Kwigize mwenyekiti TADIO na kushoto kwake ni Pelagia Kijuu mkufunzi .
Mwenye suti ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari maelezo Ndg Rodyne Mbuya akishikana mkono na Mwenyekiti wa Asasi za habari za maendeleo Tanzania Ndg Prosper Kwigize.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka radio za kijamii ambao wamepata fursa ya kutembelea Idara ya habari maelezo makao makuu Dodoma  .
Kaimu Mkurugenzi Rodyne Mbuya akisikiliza kwa makini ujio wa waandishi wa habari ,pembeni yake ni Moja ya maafisa toka Idara ya habari maelezo .
Ndg Dotto Bullendu mwanahabari nguli na mkufunzi wa maswala ya habari kutoka Chuo Kikuu cha SAUT Mwanza akizungumza jambo wakati alipojumuika na wanahabari wengine kutembelea Idara ya habari maelezo  Jijini Dodoma.
Ndg Pelagia Kijuu mkufunzi wa mafunzo ya wanahabari hao akizungumza jambo alipotembelea ofisi za Idara ya habari Maelezo  jijini Dodoma.

 

Afisa Habari wa Idara ya Habari – MAELEZO, Bi. Beatrice Lyimo akifafanua kuhusu taratibu za namna ya kupata Vitambulisho vya Waandishi wa Habari “Press Card” wakati  wa ziara ya Waandishi wa Habari wa Radio za Kijamii kwa lengo la kujifunza shughuli za Idara hiyo leo jijini Dodoma.
Namna ambavyo waandishi hawakuwa nyuma katika kuhakikisha wanachukua kila tukio lililojitokeza.
Afisa fedha na utawala -TADIO Cosmas Lupoja akifuatilia jambo kwa umakini mkubwa baada ya kutembelea ofisi ya Idara ya Habari Maelezo .
           Moja ya waandishi ambaye alipata Press card baada ya ziara .

Na Bakari Khalid

 

Dodoma

 

 

Waandishi wa habari 18 kutoka radio za kijamii leo wametembelea Idara ya habari maelezo ,kujifunza na kufahamu kwa undani shughuli za Idara hiyo .

Akizungumza kwa niaba ya wengine Mwenyekiti wa Asasi ya habari kwa maendeleo Tanzania (TADIO) Prosper Kwigize amesema wameishukuru sana idara ya habari maelezo kwa kukubali mualiko wao ,kwani ni fursa hadhimu ambayo pamoja na mambo mengine wamepata kujadili maswala mbalimbali yanayohusu taaluma ya habari.

Kwigize amesema vyombo vya habari vya kijamii vina mchango mkubwa ,hivyo ni vyema vikapewa kipaumbele kwa ndio vyombo pekee vilivyo karibu na jamii .

Akitoa malalamiko juu ya changamoto wanazokumbana nazo katika sehemu zao za kazi moja ya waandishi hao Amina Mrisho (Pambazuko FM) amesema kumekuwa na changamoto sana kwa waandishi vyombo vya kijamii kwa wanakosa  ushirikiano kwa maafisa habari wa wa mikoa.

“Wamekuwa wagumu sana kutoa ushirikiano hasa wakijua kuwa ni mwandishi habari kutoka vyombo vya kijamii” Amesema Amina .

Kwa upande wake Rodney Mbuya Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari maelezo makao makuu Dodoma,amesema amefurahishwa na ujio wa wana habari,kwani tasnia ya habari ina mchango mkubwa sana katika kufikisha taarifa kwa wananchi.

Aidha amewataka waandishi  kuwatolea taarifa kwa viongozi wao wale maafisa habari wanaokataa kutoa ushirikiano kwao,hivyo wao kama Idara kupitia wizara ya habari Sanaa utamaduni na michezo watafanyia kazi swala hilo ili wananchi waweze kupata taarifa za uhakika na kwa wakati kupitia vyombo hivyo vya kijamii kwani ndio hasa viko karibu na wananchi.

Mbuya amewataka waandishi kufanya kazi yao kwa ajili ya kizazi kijacho huku akitolea mfano taifa la china lilivyofanikiwa kwa kufanya hivyo mpaka sasa wanavuna matunda ya wazee wao.

Aidha Mbuya amewataka kuchangamkia fursa ya kupata press card ili kutambulika na Idara hiyo lakini pia itasaidia kupunguza watu wanaoichafua tasnia hiyo (kanjanja).

Jumla ya waandishi wa habari 18 kutoka radio za kijamii wapo mkoani Dodoma kwenye mafunzo ya kuwaongezea uwezo katika kuzalisha maudhui bora,Mafunzo haya yameandaliwa na TADIO kwa ufadhili wa BEST DIALOGUE.